Historia

Kanisa la Moravian lilianza shughuli zake Tanzania mwishoni mwa karne ya 19, ambapo wamisionari walianzisha kituo cha kwanza Rungwe Kusini mwa Tanzania mwaka 1891. Jimbo la Kusini-Magharibi lilianzishwa katika mwaka 1976. Jimbo limesajiliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani, lenye namba ya usajili So:6099 na hati yake ya uhalali ni namba 630. Jimbo hili limegawanyika katika wilaya tatu (3) ambazo ni, Mbeya, Chunya na Mbalizi. Pia, hufanya utume katika Iringa na Mbozi. Kiujumla jimbo linafanya maendeleo katika jamii inayoizunguka.
Jimbo linakua kwa haraka kutokana na idadi ya watu na eneo linalokaliwa. Hili ni jimbo kubwa zaidi miongoni mwa Majimbo ya Moravian. Limechukua sehemu kubwa ya utawala na kuleta changamoto za kiusimamizi, lakini jimbo la Kusini-Magharibi (SWP) bado linajiendesha kwa kutumia jina moja katika mkoa wa Mbeya.

Leo, kuna wanachama wa Moravian wapatao 215’000 katika jimbo lote, wachungaji na wainjilisti 200 wanaofanya kazi katika shirika 133, na vituo 20 vilivyo mbali na jimbo na Wachungaji wastaafu 25 ambao wanasaidiwa na jimbo. Asilimia 80 ya bajeti inatokana na vyanzo vyake (Idadi inatokana na ripoti ya 2019).

Kiswahili